SIASA TANZANIA

Peter Msigwa Amvaa Kigwangala  Amtaka Atoe Ushahidi "Nipo Tayari Kujiuzulu Nafasi Yangu ya Ubunge"

Peter Msigwa Amvaa Kigwangala Amtaka Atoe Ushahidi "Nipo Tayari Kujiuzulu Nafasi Yangu ya Ubunge"

Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa amefunguka na kuweka wazi kuwa endapo Waziri wa Maliasili na Utalii atatoa ushahidi wowote ambao unaonyesha yeye ana masilahi na makampuni ya uwindaji atajiuzulu nafasi yake ya ubunge.

Mchungaji Msigwa amesema hayo Februari 12, 2018 kupitia moja ya mitandao yake ya kijamii na kudai kuwa Waziri huyo amekuwa ni muongo na ni mtu ambaye hajiamini

"Kigwangalah ni muongo anyependa masifa, ni mtu asiyejiamini. Kama akitoa ushahidi wowote utakaodhihirisha kuwa nina masilahi na makampuni ya uwindaji nitajiuzulu ubunge .Nina wasiwasi na upbringing yake" aliandika Msigwa

Mbunge Msigwa amesema hayo kufuatia kauli ambayo Waziri Kigwangalla aliitoa siku chache zilizopita kupitia mtandao wake wa Twitter kuwa Mbunge huyo wa Iringa Mjini anahusika na ana hisa katika vitalu, jambo ambalo Msigwa mwenyewe amelipinga vikali na kuamua kuweka ubunge wake rehani endapo Waziri huyo atathibitisha hilo.
Share on Google Plus

About NASWIHEART

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Chapisha Maoni