Kocha wa Azam: Michuano Hii ni Migumu Hatutaki Kufanya Makosa
Kocha wa Azam FC Aristica Cioaba, amesema hataki timu yake ifanye
makosa kwenye mchezo wa raundi ya 16 bora ya kombe la shirikisho nchini
dhidi ya timu iliyopanda ligi kuu ya KMC.
Mchezo huo ambao unatarajiwa kupigwa jumamosi hii kwenye uwanja wa Azam
Complex, Cioaba ameueleza kuwa ni mchezo muhimu kwa timu yake kutokana
na timu hiyo kutaka kusonga mbele ya michuano hiyo.
“Hatutaki kufanya makosa na wachezaji wanafahamu michuano hii kuwa ni
migumu kama huweki umakini wa kushinda mchezo basi utapata tatizo kwa
kuwa ni mchezo mmoja tu na sio kama ligi'', amesema.
Azam FC inayoshika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi ilitinga katika
hatua hii baada ya kuifunga Shupavu ya Morogoro mabao 5-0. Wakati KMC
iliichapa Toto Africans ya Mwanza mabao 7-0.
KMC ni timu iliyopo chini ya Manispaa ya Kinondoni ya kuanzia msimu ujao
itaanza kucheza ligi kuu baada ya kufanikiwa kupanda kutoka ligi daraja
la kwanza.
0 maoni:
Chapisha Maoni