Mtulia: Kinondoni Vuteni Subira, Nakuja Tena

Jiunge na USHINDI LAZIMA kwa habari zaidi



Aliyekuwa Mbunge wa Kinondoni Dar es Salaam, Maulid Mtulia kupitia Chama cha CUF na baadaye kujiuzulu nafasi hiyo na kuhamia CCM leo Januari 17, 2018 amechukua fomu ya kuwania Ubunge katika jimbo la Kinondoni kupitia CCM

Mtulia akiongea mbele ya waandishi wa habari leo amewaomba wananchi wa jimbo hilo la Kinondoni kuwa subira na kudai ikifika wakati wa kampeni atakuwa na mambo mengi ya kuzungumza na wao. 
"Nawaambia wana Kinondoni wavute subira mpaka wakati wa kampeni ukianza nitakuwa na mambo mengi ya kusema nao lakini kwa kipindi hiki wawe watulivu kwa ajili ya kuzipokea kampeni zetu lakini vile vile kwa ajili ya kufanya maamuzi" alisema Mtulia 
Aliyewahi kuwa Mbunge wa Kinondoni jijini Dar es Salaam, Maulid Mtulia kwa tiketi ya (CUF) Disemba 2, 2017 alitangaza kujiuzulu Ubunge na kujivua uanachama wa Chama cha Wananchi CUF na kuhamia CCM kwa kile alichodai anaunga utendaji kazi wa Rais John Pombe Magufuli na serikali ya awamu ya tano.
Like kwa sana comment pamoja na kushare 


Share on Google Plus

About NASWIHEART

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Chapisha Maoni